WAJIPATIA RIZIKI KUPITIA KILIMO CHA MBUYU

Published: Nov. 29, 2021, 7:57 a.m.

Wengi hufahamu jina mabuyu yaliyozoeleka kuliwa kwa kumumunya utamu wake ambapo hupikwa kwa kuchanganya na sukari, rangi iwe ya kijani nyekundu au hata njano pamoja na viungo vyengine ambapo badae huuzwa katika paketi kati ya shilingi 5-50

\n

Lakini je unapomumunya utamu wake unafahamu pale yanapotokaa?.Yanatoka kwa mti wa m'buyu kwa kimombo baobab tree.

\n

Ni mti mkubwa wa ukanda wa tropiki na  matunda yake ndio yanaitwa mabuyu na lile gamba la tunda linaitwa kibuyu na ubuyu ndio hupikwa na kisha tunaomumunya utamu wake.

\n

Mti wa m'buyu ambao huzalisha mabuyu hustawi sana katika maeneo yenye joto ,yaliyo makavu ya Afrika na una uwezo wa kuhimili makali ya kiangazi.

\n

La zaidi ni kwamba wapo wakulima waliozama katika ukulima wa m'buyu kutokana na manufaa mengi yenye kuendeleza uhai.

\n

Wakulima hawa wanategemea mibuyu iliyopo mashambani mwao pamoja na ile iliyostawi katika msitu wa Kaya Kauma kaunti ya Kilifi.

\n

By: Mwanaharusi Rashid