Mbali na kuwa mdudu mkali wapo waliozama katika ufugaji wa nyuki kwa ajili ya uzalishaji wa asali kwa matumizi mbalimbali ikiwemo dawa.
\nIkumbukwe kuwa si wengi wenye ujasiri na ukakamavu wa kufuga nyuki kutokana na dhana na kasumba kuwa ni wadudu hatari kufuga licha ya kuwa na manufaa tele.
\nUfugaji wa nyuki hauna mahitaji mengi ikilinganishwa na ufugaji mwengine wowote cha msingi ni mfugaji kuwa na mizinga.
\nKama ukulima na ufugaji wengine wowote ule Nyuki pia hutegemea mvua kwa sababu nyuki hutegemea maua kama chakula na wakati wa mvua ufugaji wa nyuki na uzalishaji asali hushamiri.
\nBy:Mwanaharusi Rashid