Kupigania Haki za Wanawake Wenye Ulemavu Waliodulumiwa Kingono

Published: Dec. 27, 2021, 1:57 p.m.

Idadi kubwa ya wanawake wenye ulemavu wa akili,ulemavu kutosikia na ulemavu wa kuona wanapitia dhulma mbali mbali ikiwemo ubakaji katika jamii, wengi wa wanaobakwa usalia kimya wasijue wapi pa kwenda ili kupiga ripoti angalau wapate haki zao za kisheria.

\n

Jijini Mombasa Pwani ya Kenya shirika la \u201cTunaweza Women With Disability\u201d limeanza kutoa usaidizi wa kisheria na mafunzo mbali mbali kwa wanawake wenye ulemavu sawia na wazazi wenye watoto walemavu ili waweze kuzinduka na kupigania haki zao.

\n

By:Athuman Luchi