Kifafa Siyo Uchawi

Published: Jan. 31, 2023, 8:20 p.m.

Kifafa ni ugonjwa wa ubongo unaosababisha mtu kupoteza fahamu kwa muda.

\n

Ugonjwa huu unaweza kumsababishia mtu kufanya vitendo visivyokuwa vya kawaida kama vile kuanguka, kufifitika na hata baadhi ya wagonjwa kutojielewa.

\n

Kulingana na takwimu kutoka kwa shirika la afya dunia WHO, takriban watu milioni 50 duniani wanaugua maradhi haya, na kuyafanya kuwa miongoni mwa maradhi maarufu zaidi ya ubongo duniani.