Maendeleo kidogo katika mazungumzo ya mkataba wa kukomesha uchafuzi wa plastiki

Published: Nov. 21, 2023, 8:13 a.m.

Msikilizaji kwa juma moja, wajumbe kutoka mataifa takriban 175, walikusanyika jijini Nairobi kwa majadiliano ya awamu ya tatu kuelekea kuundwa kwa mkataba wa kisheria wa kimataifa kupambana na uchafuzi utokanao na taka za plasitki ikiwa ni pamoja na mazingira ya baharini.

Katika kipindi hiki, wajumbe wa serikali na wadau wengine kutoka mashirika yasio ya kiserikali walikuwa wakijadili mapendekeo ya maudhui yanayofaa kujumuishwa kwenye mkataba huo wa kisheria.

 

Baadhi ya nchi zimependekeza mkataba huo kuangazia matumizi endelevu ya bidhaa za plastiki kuanzia kwenye uzalishaji hadi matumizi yake, huku zingine zikipendelea mkataba huo kuangazia suala la uchakataji na matumizi ya tena ya plastiki.

Kwa kuanza makala yetu hivi leo, tunaye Henry Msuya, mjumbe wa Tanzania kwenye majadiliano ya mktababa wa kudhibiti taka za plastiki. Hapa anaanza kwa kueleza namna majadiliano yalivyokuwa wiki nzima.